Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » MAYASA MRISHO AOLEWA KINYEMELA

MAYASA MRISHO AOLEWA KINYEMELA


TETESI zilizopo mtaani ni kwamba msanii wa filamu, Mayasa Mrisho ‘Maya’ ameolewa kwa siri na katika kuthibitisha hilo, mwanadada huyo sasa hivi anavaa pete ya uchumba na ya ndoa.

Rafiki wa karibu wa msanii huyo aliyeomba hifadhi ya jina lake alidai kuwa, alichokuwa akijua ni kwamba Maya ana mchumba lakini siku za hivi karibuni ameshangazwa na hatua ya kuolewa kwake kwa siri.

“Mi’ nakwambieni ukweli nina uhakika Maya kaolewa, kama hamuamini mtazameni kidoleni anayo pete ya ndoa na ya uchumba,” kilidai chanzo hicho.

Katika kufuatilia ilibainika kuwa ni kweli msanii huyo anavaa pete hizo na alipoulizwa juu ya taarifa hizo za kuolewa kwa siri alisema:

“Jamani nyie eleweni tu mchumba ninaye lakini bado sijaolewa ila kaeni tayari siku yoyote na mimi nitaitwa Mrs flani."
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK

Translate

 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. MPEKUZI - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger